Wednesday, June 14, 2017

LEICESTER YANASA BEKI KUTOKA HULL CITY.

KLABU ya Leicester City inatarajiwa kutangaza usajili wa beki wa Hull City Harry Maguire ambao umewagharimu kiasi cha paundi milioni 17. Taarifa kutoka nchini Uingereza zinadai kuwa Leicester wanatarajia kutoa paundi milioni 12 mwanzo huku nyingine ikitarajiwa kulipwa kwa makubaliano na tayari nyota huyo ameshakamilisha vipimo vya afya. Maguire mwenye umri wa miaka 24, alifunga mabao matatu katika mechi 36 alizoichezea Hull City iliyoteremka daraja msimu uliopita. Beki huyo wa kati ambaye alijiunga na Hull City kwa kitita cha paundi milioni 2.5 akitokea Shiffield United mwaka 2014 alikuwa amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wake.

No comments:

Post a Comment