Wednesday, June 14, 2017

LINDELOF ATUA OLD TRAFFORD KUKAMILISHA USAJILI WAKE.

BEKI wa kimataifa wa Sweden, Victor Lindelof ametua katika uwanja wa mazoezi wa Manchester United kuelekea kukamilisha uhamisho wake wa paundi milioni 30. United imethibitisha kuwa tayari kumsajili beki huyo, ambaye atakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Jose Mourinho kipindi hiki cha majira ya kiangazi. Lindelof amewasili katika uwanja wa mazoezi wa United wa AON kufanyiwa vipimo vya afya ili kukamilisha usjaili wake kutoka Benfica ya Ureno. Taarifa zinadai kuwa Lindelof amekubali mkataba wa miaka minne Old Trafford huku kukiwa na kipengele cha kuongezewa.

No comments:

Post a Comment