Monday, June 19, 2017

LIVERPOOL YAMUWANIA AUBAMEYANG.

TAARIFA kutoka nchini Ufaransa zinadai kuwa Liverpool inajipanga kumuwania mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang. Taarifa hizo zimeongeza kuwa Jurgen Klopp anafikiria kuungana tena na mashambuliaji huyo Anfield baada ya kuwahi kumfundisha wakati wakiw ote Dortmund. Liverpool inajipanga kuimarisha kikosi chake kwa kiasi kikubwa kutokana na ushiriki wao katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao na tayari Aubameyang alishaeleza nia yake ya kuondoka Dortmund kama ofa sahihi ikipatikana. Aubameyang alifunga mabao 42 kwa klabu na nchi yake msimu uliopita na ni mmoja kati ya washambuliaji wanaohofiwa barani Ulaya.

No comments:

Post a Comment