Monday, June 19, 2017

PEREZ KUENDELEA KUWA RAIS WA MADRID.

RAIS wa Real Madrid, Florentino Perez anatarajia kuendelea na wadhifa wake huo mpaka mwaka 2021 baada ya kutojitokeza mgombea yeyote wa kugombea nafasi hiyo. Perez ambaye mara ya kwanz akushika wadhifa huo ilikuwa ni mwaka 2000, amefanikiwa kupita bila kupingwa katika taarifa iliyotolewa na mabingwa hao wa Hispania na Ulaya mapema leo. Perez mwenye umri wa miaka 70 ameendelea kuchagiza mafanikio katika klabu hiyo baada ya kutwaa taji la tatu la michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya katika kipindi cha misimu minne iliyopita. Madrid pia walifanikiwa kutwaa taji la La Liga kwa mara ya kwanza toka mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment