Friday, June 23, 2017

MAPETO YA NGAO YA HISANI UINGEREZA KWENDA KWA WAATHIRIKA WA MOTO.

MAPATO kutoka katika mchezo wa Ngao ya Hisani nchini Uingereza mwaka huu yanatarajiwa kutolewa kwa ajili ya waathirika wa moto katika jingo la Grenfell Tower. Arsenal wanatarajiwa kucheza na Chelsea Agosti 6 mwaka huu katika Uwanja wa Wembley na kiasi cha paundi milioni 1.25 kinatarajiwa kukusanywa katika mchezo huo. Mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Uingereza-FA, Greg Clarke amesema wana matumaini kiasi hicho kidogo watakachopata kupitia mchezo wa Ngao ya Hisani kinaweza kusaidia waathirika hao. Clarke amesema mchezo wa soka ni wa wote wana matumaini kwa njia zake yenyewe itaweza kurudisha hisani hiyo kidogo kwa wale wanaohitaji zaidi. Watu waliosalimika, familia za wahanga na watu waliotoa msaada wa dharura wanatarajiwa kualikwa katika mchezo huo kama wageni rasmi.

No comments:

Post a Comment