Thursday, June 22, 2017

NDUGU WA MBAPPE AELEZA NDUGUYE ANAWEZA KWENDA ARSENAL.

NDUGU wa karibu wa Lylian Mbappe amekiri nyota huyo wa Monaco anaweza kujiunga na Arsenal kipindi hiki cha majira ya kiangazi na kusisitiza kutokuwepo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa kwa klabu hiyo sio tatizo. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger alikaribia kumsajili Mbappe kiangazi mwaka jana lakini mshambuliaji huyo aliamua kubakia kwa mwaka mwingine zaidi. Nyota huyo ambaye amefunga mabao 26 msimu uliopita amezivutia klabu kubwa barani Ulaya zikiwemo Real Madrid na Barcelona. Awali ilikuwa ikihofiwa kuwa kushindwa kwa Arsenal kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya kunaweza kuwanyima nafasi ya kumsajili nyota huyo.

No comments:

Post a Comment