Thursday, June 15, 2017

SOUTHAMPTON WAMTIMUA KOCHA WAO.

KLABU ya Southampton imemtimua rasmi meneja wake Claude Puel baada ya kuinoa timu hiyo kwa msimu mmoja. Meneja huyo mwenye umri wa miaka 55 raia wa Ufaransa, ambaye aliteuliwa kushika nafasi hiyo Juni mwaka jana, aliiongoza Southampton kushika nafasi ya nane katika msimamo wa Ligi Kuu msimu uliopita pamoja na kupotez amechi 16. Southampton pia ilifanikiwa kutinga fainali ya Kombe la Ligi ikiwa ni fainali yao ya kwanza kubwa toka mwaka 2003. Katika taarifa ya klabu hiyo imedai kuwa mchakato wa kutafuta kocha mpya tayari umeanza na wana uhakika watapata chaguo sahihi. Puel aliinoa Nice kwa mwaka mmoja kabla ya kuja kuchukua nafasi ya Ronald Koeman aliyeingoza Southampton kushika nafasi ya sita katika msimamo wa ligi msimu wa 2015-2016.

No comments:

Post a Comment