Monday, June 19, 2017

WILSHERE "AVUTA JIKO".

KIUNGO wa Arsenal, Jack Wilshere amefunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi Andriani Michael katika sherehe kubwa ya siku tatu iliyofanyika nchini Italia. Wilshere alituma picha akiwa na mpenzi wake huyo kwenye harusi katika mitandao ya kijamii huku kukiwa na ujumbe wa kuwashukuru wale wote walioshirikiana naye kwenye siku yake hiyo muhimu. Wawili hao walifunga ndoa huko Tuscany, huku mwanamuziki nyota wa Uingereza Graig David akitumbuisha katika sherehe hizo. Sherehe hiyo ilihudhuriwa na familia pamoja na marafiki zake wa karibu akiwemo Benik Afobe, Wjciech Szczesny, Danny Welbeck na Dan Crowley ambao wote amecheza nao Arsenal.

No comments:

Post a Comment